Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Katiba na Sheria

Tathmini ya Ukarabati Jengo La Usuluhishi Ikamilike Kwa Wakati

Imewekwa: 07 Jul, 2024
Tathmini ya Ukarabati Jengo La Usuluhishi Ikamilike Kwa  Wakati

Hyasinta Kissima – WKS Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini Julai 6, 2024 akiwa ameambatana na baadhi ya Wakurugenzi  kutoka Wizara ya Katiba na Sheria wametembelea katika jengo linalotarajiwa kutumika kuwa Kituo cha Usuluhishi kilichopo Temeke,  jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri Sagini ameelekeza kuharakishwa kwa kazi ya kufanyika kwa  tathmini ya ukarabati wa jengo hilo inayofanywa na TBA ili ukarabati ukamilike kwa wakati na jengo hilo lianze kutumika.

Aidha, Mhe. Sagini ameelekeza Sekretarieti ya Kituo cha Usuluhishi kianze kuandaliwa mapema ili jengo litakapokuwa limekamilika lianze kufanya kazi mara moja.