Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Katiba na Sheria

Historia ya Wizara

Wizara ya Katiba na Sheria ndiyo mhimili mkuu wa masuala yote ya kisheria nchini. Bila shaka ni kutokana na umuhimu huu, ndiyo sababu Wizara hii ikawa na umri wa miaka 55 sawa na umri nchi yetu hii leo.

Historia ya Wizara ilianza mwaka 1961 wakati Waziri Mkuu wakati huo, Hayati Julius Nyerere alipomteua Chifu Abdallah Fundikira kuwa Waziri wa Sheria wa Kwanza Mzalendo kabla nafasi hiyo kuchukuliwa na Sheikh Amri Abeid Kaluta mwaka 1963 na baadaye Mhe. Hassan Nassor Moyo kuanzia mwaka 1964 aliyeshika nafasi hiyo hadi 1966. Baada ya hapo shughuli za Wizara zilihamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu na Makamu wa Pili wa Rais chini Hayati Rashid Mfaume Kawawa.

Baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1975, Wizara na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ziliunganishwa kupitia Tangazo la Serikali Na. 10 la mwaka 1975 na Mhe. Jullie Manning aliteuliwa kuwa Waziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali hadi mwaka 1982 alipoteuliwa Mhe. Joseph Warioba kushika nafasi hizo. Utaratibu huu uliendelea hata baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1985 wakati Mhe. Damian Lubuva alipoteuliwa kushika nyadhifa hizo mbili hadi mwaka 1990.

Mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri yaliyofanywa mwaka 1990 yalipelekea Waziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutenganishwa tena na hivyo kofia ya Uwaziri na kofi ya Uanasheria Mkuu wa Serikali zikatofautishwa. Wakati huo, shughuli za Waziri zilihamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ikabaki kuwa Idara inayojitegemea chini ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais. Mabadiliko haya yalifanywa kupitia Tangazo la Serikali Na. 140 la mwaka 1990.

Mwaka 1993, Rais Alli Hassan Mwinyi aliirudisha tena Wizara ya Sheria na Mambo ya Katiba na kumteua Mhe. Samuel Sitta kuwa Waziri na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ikabaki kuwa Idara inayojitegemea chini ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais.

Baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995, Rais Benjamin Mkapa aliendelea na Wizara hii kupitia Tangazo la Serikali Na. 720 la mwaka 1995 na kumteua Mhe. Harith Mwapachu kuwa Waziri. Katika muundo huu mpya, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ilirudishwa chini ya Wizara hii kutoka Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais na Katibu Mkuu wa Wizara akawa pia ndiye Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Mwaka 2005, baada ya Uchaguzi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete aliunda tena Wizara hii wakati huu ikiitwa Wizara ya Katiba na Sheria. Hata hivyo, ili kuongeza ufanisi, mwaka 2008 kufuatia mapendekezo ya Tume ya Jaji Mark Bomani, Wizara ilitenganishwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali hatua iliyopelekea pia kutenganishwa kwa nafasi ya Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali na ile ya Katibu Mkuu wa Wizara.

MAWAZIRI WA SHERIA 1961 - 2022

Mwaka

Jina la Waziri

Jina la Wizara

1961 – 1963

Mhe. Chifu Abdallah Said Fundikira (Mb)

Waziri wa Mambo ya Sheria

1963 – 1964

Mhe. Sheikh Amri Abeid Kaluta (Mb)

Waziri wa Sheria

1964 – 1966

Mhe. Hassan Nassor Moyo (Mb)

Waziri wa Sheria

1966 – 1975

Mhe. Rashid Mfaume Kawawa (Mb)

Waziri Mkuu na Makamu wa Pili wa Rais

1975 – 1982

Mhe. Julie Manning (Mb)

Waziri wa Sheria

1982 – 1985

Mhe. Joseph Warioba (Mb)

Waziri wa Sheria na Mwanasheria Mkuu wa Serikali

1985 – 1990

Mhe. Damian Lubuva (Mb)

Waziri wa Sheria na Mwanasheria Mkuu wa Serikali

1990 – 1990

Mhe. Joseph Warioba (Mb)

Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais

1990 – 1993

Mhe. John Malecela (Mb)

Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais

1993 – 1995

Mhe. Samwel Sitta (Mb)

Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba

1995 – 2005

Mhe. Harith Bakari Mwapachu (Mb)

Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba

2006 – 2008

Mhe. Dkt. Mary Nagu (Mb)

Waziri wa Katiba na Sheria

2008 – 2010

Mhe. Mathias Chikawe (Mb)

Waziri wa Katiba na Sheria

2010 – 2012

Mhe. Celina Kombani (Mb)

Waziri wa Katiba na Sheria

2012- 2014

Mhe. Mathias Chikawe (Mb)

Waziri wa Katiba na Sheria

2014 -2015

Mhe. Dkt Asha Rose Migiro (Mb)

Waziri wa Katiba na Sheria

2015 -2017

Mhe.Dkt Harrison George Mwakyembe (Mb)

Waziri wa Katiba na Sheria

2017- 2019

2019- 2020

2020 - 2021

2021 - 2022

2022 - 2022

2022 hadi sasa

Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (Mb)

Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb)

Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb)

Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (Mb)

Mhe. George Simbachawene (Mb)

Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb)

Waziri wa Katiba na Sheria

Waziri wa Katiba na Sheria

Waziri wa Katiba na Sheria

Waziri wa Katiba na Sheria

Waziri wa Katiba na Sheria

Waziri wa Katiba na Sheria

MAKATIBU WAKUU 1961 - 2022

Mwaka

Jina

Cheo

1961-1964

Ndg. David Levric DAVIES,O.B.E

Katibu Mkuu na Wakili Mkuu wa Serikali

1964-1965

Ndg. Mark D. BOMANI

Katibu Mkuu na Wakili Mkuu wa Serikali

1975-1987

Ndg. Damian S. Meela

Katibu Mkuu na Naibu Mwanasheria Mkuu

1987-1991

Ndg. T.L. Mkude

Katibu Mkuu na Naibu Mwanasheria Mkuu

1991-1993

Ndg. Andrew Chenge

Katibu Mkuu na Naibu Mwanasheria Mkuu

1993-1997

Ndg. Felix Mrema

Katibu Mkuu na Naibu Mwanasheria Mkuu

1997-2002

Ndg. Kulwa Masaba

Katibu Mkuu na Naibu Mwanasheria Mkuu

2002-2005

Ndg. Johnson P.M Mwanyika

Katibu Mkuu na Naibu Mwanasheria Mkuu

2006-2008

Ndg. Vincent D.Lyimo

Katibu Mkuu na Naibu Mwanasheria Mkuu

2008 -2009

Ndg. Sazi B. Salula

Katibu Mkuu na Naibu Mwanasheria Mkuu

2009 – 2011

Ndg. Oliver P.J. Mhaiki

Katibu Mkuu

2011 - 2014

Ndg. Fanuel Mbonde

Katibu Mkuu

2014 - 2015

Ndg. Maimuna Tarishi

Katibu Mkuu

2016 - 2022

2022 hadi sasa

Prof. Sifuni Ernest Mchome

Ndg. Mary Makondo

Katibu Mkuu

Katibu Mkuu