Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Katiba na Sheria

Kitengo cha TEHAMA

Malengo:

Kutoa utaalamu wa huduma za matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mmawasiliano (TEHAMA)  kwa Wizara.

Kitengo hiki kinatekeleza shughuli zifuatazo:

  1. Kutekeleza uendelezaji wa TEHAMA pamoja na Sera ya Serikali Mtandao;
  2. Kuandaa na kuratibu Maunganisho ya Teknolojia yaHabari na Mawasiliano Wizarani;
  3. Kuhakikisha Hardware na Software zinatunzwa vyema;
  4. Kuratibu na kutoa ushauri  wa Kitaalam katika ununuzi wa Software na Hardware za Wizara;
  5. Kuanzisha na kuratibu matumizi ya mawasiliano ya Barua Pepe, Locala Area Network na Wide Area Network;
  6. Kubuni, kuendeleza, kusimika, kusimamia na kutunza miundombinu ya TEHAMA na mifumo ya habari  na mawasiliano kwa kushirikiana na Mamlaka ya Serikali Mtandao;
  7. Kuandaa na kutekeleza mpango wa huduma endelevu  kw aWizara;
  8. Kutoa ushauri wa kiufundi kuhusu mifumo na miundombinu  ya TEHAMA ya Wizara;
  9. Kutoa huduma na usaidizi kwa watumiaji;
  10. Kuratibu uhifadhi wa data;
  11. Kutekeleza huduma za usalama za TEHAMA; na
  12. Kufanya tafiti na kupendekeza maeneo ya kutumia TEHAMA kama chombo cha kuboresha utoaji wa huduma kwa Wizara;

       Kitengo kinaongozwa na Mkuu wa Kitengo