Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, akiwasikiliza na kuwahudumia wananchi kupitia programu ya ''Sema na Waziri'', iliyoendeshwa kupitia Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Wizara, 22 Machi, 2026, Mtumba, jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera (wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na baadhi ya wakurugenzi na wataalam wa sheria mara baada ya kuwasikiliza na kuwahudumia wananchi kupitia programu ya ''Sema na Waziri'', iliyoendeshwa kupitia Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Wizara, 22 Machi, 2026.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka wa fedha 2026/2027 itasomwa Bungeni jijini Dodoma, tarehe 24 Aprili, 2026,
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, akizunguza na watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wakati akifunga rasmi mafunzo elekezi ya watumishi hao (waajiriwa wapya), 19 Aprili, 2026 Jijini Arusha.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Athuman Katimba (Mb.), akifungua rasmi mafunzo ya awali kwa waajiriwa wapya 162 wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka yanayofanyika jijini Arusha tarehe 15 Aprili 2026.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera (wa Pili kulia) akikata utepe kuashiria kukabidhi magari 5 kwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bw. Patience Ntwina (Kulia kwake) wakati wa hafla ya kukabidhi magari na vitendea kazi kwa Mahakama ya Tanzania,15 Aprili, 2026 Mtumba Jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Juma Homera (kushoto) akikabidhi Kompyuta Mpakato kwa Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Bi. Eva Nkya wakati wa hafla ya kukabidhi Magari na Vitendea kazi kwa Mahakama ya Tanzania na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora 15 Aprili, 2026, Mtumba Jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Juma Homera (kushoto) akikabidhi vitendea kazi (Kompyuta Mpakato) kwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bw. Patience Ntwina wakati wa hafla ya kukabidhi Vitendea kazi kwa Mahakama ya Tanzania na Tume hiyo 15 Aprili, 2026, Mtumba Jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, akisikiliza na kuwahudumia wananchi waliopiga simu katika Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Wizara, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa programu ya ''Sema na Waziri'' tarehe 15 Machi, 2026, Mtumba jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera (kulia) akiwa katika mahojiano kuhusiana na programu ya ''Sema na Waziri'' kupitia kipindi cha Clouds 360, mahojiano mubashara yamefanyika katika Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Wizara, Mtumba jijini Dodoma, tarehe 15 Machi, 2026.