Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, akiwasikiliza na kuwahudumia wananchi wakati wa programu ya ''Sema na Waziri'', inayoendeshwa kupitia Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Wizara, 7 Mei, 2026, Mtumba, Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Zainab Athuman Katimba, akijibu swali kuhusu hatua zinazochukuliwa na serikali katika kuimarisha taasisi ya ndoa na kushughulikia migogoro ya kifamilia, wakati wa shughuli za Bunge la Kumi na Tatu, Mkutano wa Tatu, Kikao cha Ishirini na Nne, 07 Mei, 2026, Bungeni, jijini Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Utatuzi wa Migogoro kwa njia mbadala wa Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Felix Chakila akifungua rasmi mafunzo maalum kwa wasuluhishi na waamuzi kutoka mikoa mbalimbali nchini kwa lengo la kuimarisha matumizi ya mbinu mbadala za utatuzi wa migogoro (ADR) ili kuhakikisha mazingira salama na yenye tija mahali pa kazi, jijini Dar es Salaam, 5 Mei, 2026.
Washiriki wa mafunzo maalum ya wasuluhishi na waamuzi kutoka mikoa mbalimbali nchini, wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo yenye lengo la kuimarisha matumizi ya mbinu mbadala za utatuzi wa migogoro (ADR) katika kuhakikisha mazingira salama na yenye tija mahali pa kazi, 5 Mei, 2026, jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, akifungua rasmi Mkutano Mkuu wa 11 wa Umoja wa Waendesha Mashtaka Ukanda wa Afrika Mashariki, uliofanyika jijini Dar es Salaam, 4 Mei, 2026.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Athuman Katimba, akizungumza jambo wakati wa Mkutano Mkuu wa 11 wa Umoja wa Waendesha Mashtaka Ukanda wa Afrika Mashariki, uliofanyika jijini Dar es Salaam, 4 Mei, 2026.
Baadhi ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa 11 wa Umoja wa Waendesha Mashtaka Ukanda wa Afrika Mashariki, wakati wa mkutano huo uliofanyika katika jijini Dar es Salaam, 4 Mei, 2026.
Wafanyakazi Hodari wa Wizara ya Katiba na Sheria, katika picha ya pamoja mara baada ya kupokea vyeti vya pongezi kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani, ambapo kitaifa yaliongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Mkoani Njombe leo, 1 Mei, 2026.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Juma Homera (wa pili kulia) akiwasili katika viwanja vya Lunyanywi Mkoani Njombe kwaajili ya kushiriki maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Wafanyakazi leo, 1 Mei, 2026
Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria, wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, ambapo kwa Mkoa wa Dodoma yamefanyika katika Uwanja wa Jamhuri, 1 Mei, 2026.