Mkurugenzi wa Katiba na Ufuatiliaji Haki kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Jane Lyimo, akifungua rasmi wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa Uchunguzi na Upelelezi tarehe 13 Aprili, 2026, jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Katiba na Ufuatiliaji Haki kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Jane Lyimo (katikati) katika picha ya pamoja na wawezeshaji na baadhi ya maafisa Uchunguzi na Upelelezi baada ya ufunguzi rasmi wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa Uchunguzi na Upelelezi tarehe 13 Aprili, 2026, jijini Dodoma.
Baadhi ya Maafisa Uchunguzi na Upelelezi wakiwa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa kwa lengo la kuimarisha mnyororo wa haki jinai nchini. Mafunzo yanafanyika kwa siku nne tarehe 13-16 Aprili 2026, jijini Dodoma.
Kaimu Mkurugenzi Kitengo cha Uangalizi wa Utajiri Asili na Maliasilia kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Everest Mashiba, akifungua rasmi mafunzo ya kuimarisha uelewa katika usimamizi na ulinzi wa rasilimali za Taifa, 31 Machi, 2026.
Picha ya pamoja ya watumishi kutoka Wizara ya Katiba na Sheria na Taasisi za Kisekta wakati wa mafunzo ya kuimarisha uelewa katika usimamizi na ulinzi wa rasilimali za Taifa, mafunzo yanafanyika Mjini Morogoro kuanzia tarehe 30 Machi hadi 2 Aprili, 2026.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, akifuatilia uwasilishwaji wa makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge kwa mwaka wa fedha 2026/27, katika kikao cha pili cha mkutano wa tatu wa Bunge la 13, tarehe 1 Aprili, 2026, Bungeni jijini Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Edwin Enosy Swalle (Mb) akijadili jambo wakati wa kikao cha uwasilishaji wa Randama ya Mpango na Bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka wa fedha 2026/2027, 28 Machi, Bungeni, jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera (kulia) na Naibu Waziri Mhe. Zainab Athuman Katimba (kushoto) wakifuatilia jambo wakati wa kikao cha uwasilishaji wa Randama ya Mpango na Bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2026/2027 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uawala, Katiba na Sheria (hawapo pichani), 28 Machi, 2026, Bungeni jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Eliakim Chacha Maswi, akichangia jambo wakati wa kikao cha uwasilishaji wa Randama ya Mpango na Bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2026/2027 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uawala, Katiba na Sheria (hawapo pichani), 28 Machi, 2026, Bungeni jijini Dodoma.
Baadhi ya Viongozi wa Wizara ya Katiba na Sheria na Taasisi zilizo chini ya Wizara, wakiongozwa na Waziri Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, wakifuatilia kwa makini kikao cha uwasilishaji wa Randama ya Mpango na Bajeti ya Wizara 2026/2027 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uawala, Katiba na Sheria, 28 Machi, 2026, Bungeni jijini Dodoma.