Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi (wa kwanza kushoto), akipata maelezo mafupi kutoka kwa Mkurugenzi wa Huduma za Msaada wa Kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Ester Msambazi, alipotembelea banda la wizara wakati wa uzinduzi rasmi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Awamu ya Pili, 20 Juni, 2026.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Athuman Katimba, akifuatilia uzinduzi rasmi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Awamu ya Pili, uliofanyika kitaifa katika uwanja wa Dole Kizimbani, Zanzibar, 20 Juni, 2026.
Wananchi wa Zanzibar wakiwa katika uwanja wa Dole Kizimbani kushuhudia uzinduzi rasmi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Awamu ya Pili, 20 Juni, 2026.
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Alfred Dede (katikati) katika picha ya pamoja na wataalam wa wizara alipotembelea banda la wizara hiyo katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma, 18 Juni, 2026.
Baadhi ya wananchi waliotembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma wakipata huduma kutoka kwa mtaalam, 18 Juni, 2026, katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. John Jingu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Haki Jinai ngazi ya Makatibu wakuu akiongoza kikao cha Jukwaa hilo kilichofanyika Mtumba Jijini Dodoma, 10 Juni, 2026, pembeni yake ni Mkurugenzi wa Katiba na Ufuatiliaji Haki kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Jane Lyimo.
Katibu Mkuu, Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. John Jingu (katikati) katika picha ya pamoja na wajumbe wa Jukwaa la Haki Jinai ngazi ya Makatibu wakuu kutoka katika wizara na taasisi mbalimbali zilizo chini ya mnyororo wa haki jinai mara baada ya kikao cha jukwaa hilo, kilichofanyika Mtumba Jijini Dodoma, 10 Juni, 2026.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Franklin Jasson Rwezimula (katikati) katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa mafunzo mara baada ya kufungua rasmi mafunzo ya kulinda, kukuza na kutetea haki za watu wenye ulemavu, 8 Juni, 2026, Morena, Jijini Dodoma.
Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Gowele (Katikati), katika picha ya pamoja na viongozi wa Chama wa Waandishi wa Habari Wilaya ya Tarime baada ya kufungua rasmi Mafunzo ya waandishi wa habari kuhusu upatikanaji haki kupitia huduma za msaada wa kisheria, 8 Juni, 2026, Tarime.
Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Athumani Msosole akitoa elimu ya Msaada wa Kisheria kwa waandishi wa habari kutoka katika Wilaya ya Tarime, 8 Juni, 2026.