Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Franklin Jasson Rwezimula (katikati), Kaimu Balozi wa Ujerumani Nchini Manuel Muller (wa pili kushoto), Mkurugenzi Huduma za Msaada wa Kisheria Wizara ya Katiba na Sheria Ester Msambazi (wa pili kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na watoa huduma za msaada wa kisheria mara baada ya kukamilika kwa hafla ya kufunga Mradi wa Jamii Kuchukua Hatua kwa Usawa (SAFE) na Mradi wa Kukuza Utawala wa Sheria na Mahakama Barani Afrika (ProLA) tarehe 16 Juni, 2026 jijini Dar es Salaam.
Jaji Mkuu wa Tanzania,Mhe. George Masaju akimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt.Seif Shekalaghe, wakati alipomtembelea katika makao makuu ya Mahakama, Tambukareli jijini Dodoma Julai 15, 2026
Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBU) Bw. Patience Ntwina (kushoto), akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Msaidiizi Sehemu ya Usuluhishi wa Migogoro, Bw. Felix Chakila, alipotembelea Banda la Wizara ya Katiba na Sheria kwa lengo la kujionea namna huduma za kisheria zinavyotolewa kwa wananchi, wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara, yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam, 10 Julai, 2026.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Athuman Katimba (wa kwanza kulia), akishiriki hafla ya uapisho wa kuwakubali na kuwapokea mawakili wapya 655, iliyofanyika katika viwanja vya Mahakama Kuu ya Tanzania, jijini Dodoma, 9 Julai, 2026.
Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) katika picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama za Tanzania wakati wa hafla ya uapisho wa kuwakubali na kuwapokea mawakili wapya 655, iliofanyika katika viwanja vya Mahakama Kuu ya Tanzania, jijini Dodoma, 9 Julai, 2026, wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Athuman Katimba ambaye pia alishiriki katika hafla hiyo.
Baadhi ya Wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Katiba na Sheria wakiendelea kupata huduma kutoka kwa wataalam wa wizara wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam, 9 Julai, 2026.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Alice Mtulo (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Usuluhishi, Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Felix Chakila, wakati alipotembelea banda la wizara wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara, yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam, 6 Julai, 2026.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Alice Mtulo, akipata maelezo ya huduma za kisheria zinazotolewa na wataalam wa wizara wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara, yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam, kutoka kwa Afisa Sheria, Bi. Tuma Gwitekere, 6 Julai, 2026.
Baadhi ya wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Katiba na Sheria lililopo katika viwanja vya Mwalimu Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam wakiendelea kupata huduma mbalimbali kutoka kwa wataalam wa Wizara, 6 Julai, 2026.
Kamishina Jenerali wa Idara ya Uhamiaji Nchini, CGI Dkt. Anna Makakala (kushoto), ametembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria na kujionea namna wizara inavyotoa huduma za kisheria kwa wananchi wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara, yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam, 6 Julai, 2026.