Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera akishiriki katika Mkutano wa Ngazi ya Juu ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa unaofanyika Nchini Geneva, Uswisi, tarehe 23-24 Februari, 2026.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Zainab Katimba (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Kikosi Kazi cha Ulinzi wa Mtoto ghidi ya biashara ya haramu ya usafirishaji wa binadamu mara baada ya kutembelea ofisi za Kikosi Kazi hicho na kupokea taarifa ya utendaji kazi, leo tarehe 23 Februari, 2026, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Zainab Katimba ametembelea Ofisi inayotumiwa na Kikosi kazi cha Ulinzi wa mtoto dhidi ya biashara haramu ya usafirishaji wa binadam na kukagua miundo mbinu ya kidigitali inayotumiwa na kikosi kazi hicho katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku, tarehe 23 Februari, 2026 Jijini Dar Es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Eliakim Maswi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Chama cha Mawakili wa Afrika Mashariki mara baada ya kukamilika kwa mazungumzo baina ya pande mbili ambapo Chama hicho kiliongozwa na Katibu, Wakili John Seka (wa tatu kulia) tarehe 20 Februari, 2026, Mtumba, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Maswi (katikati), katika picha ya pamoja na Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), Prof. Charles Kihampa (wa tatu kutoka kulia), Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe anayeshughulikia Taaluma, Utafiti na Ushauri, Prof. Hawa Tundui (wa tatu kutoka kushoto), wahadhiri kutoka kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu Mzumbe,pamoja na Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria baada ya kikaocha kujadili mikakati ya kuboresha sekta ya Sheria nchini, hususan katika ngazi ya vyuo vikuu, tarehe 12 Februari, 2026.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Maswi, akiongoza kikao cha kujadili mikakati ya kuboresha sekta ya Sheria nchini, hususan katika ngazi ya vyuo vikuu, kikao kilihudhuriwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), Prof. Charles Kihampa pamoja na wahadhiri wa kitivo cha Sheria Chuo Kikuu Mzumbe na menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria (hawapo pichani), tarehe 12 Februari,2026, Mtumba jijini Dodoma.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), Prof. Charles Kihampa akichangia jambo wakati wa kikao cha kujadili mikakati ya kuboresha sekta ya Sheria nchini, hususan katika ngazi ya vyuo vikuu, kikao kilifanyika katika ofisi za Wizara ya Katiba na Sheria, tarehe 12 Februari,2026, Mtumba jijini Dodoma.
Kwa changamoto zote za kisheria wasiliana nasi kupitia kituo chetu cha Huduma kwa Mteja
Mkurugenzi wa Katiba na Ufuatiliaji Haki kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Jane Lymo (kushoto) akimuelezea Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera (kulia) namna Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Wizara kinavyofanya kazi katika kuwahudumia wananchi, wakati ambapo waziri alitembelea kituo hicho, 5 Februari, 2026, Mtumba jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Gabriel Omar, akimuelezea Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera (hayupo pichani), namna Mifumo ya TEHAMA ya Wizara inavyotoa huduma za kisheria kwa wananchi, 5 Februari, 2026 Mtumba, jijini Dodoma