Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (katikati) kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maveterani waliopigana vita ya Uganda wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa kwenye Viwanja vya Mashujaa eneo la Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma. Mgeni Rasmi katika Maadhimisho hayo alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Julai 25, 2024.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi. Dkt. Pindi Chana alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Switzerland aliyemaliza muda wake nchini Tanzania Bw. Didier Chasot. Julai 22, 2024 Dar es Salaam.
Balozi wa Switzerland aliyemaliza muda wake nchini Tanzania Bw. Didier Chasot akifanya mazungumzo na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi. Dkt. Pindi Chana. Julai 22, 2024 Dar es Salaam.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi. Dkt. Pindi Chana na Balozi wa Switzerland aliyemaliza muda wake nchini Tanzania Bw. Didier Chasot kwenye picha ya pamoja na baadhi ya maofisa kutoka ofisi hizo mbili baada ya kufanya mazungumzo. Julai 22, 2024 Dar es Salaam.
Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiendelea na mafunzo ya Usimamizi wa Vihatarishi "Risk Management," Julai 18, 2024 Ofisi za Wizara Mtumba, Dodoma.
Msajili wa Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria Bi. Ester Msambazi akiwasilisha rasimu ya daftari la orodha ya watoa huduma wa Msaada wa kisheria kwa wadau walioshiriki uboreshaji wa Daftari la Orodha ya Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria. Julai 16, 2024 Dodoma.
Mdau Maiko Salali kutoka asasi ya Foundation for Disability Hope akichangia katika mjadala wa kuboresha Daftari la Orodha ya Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria leo tarehe 16/07/2024.
Leonard Haule ambaye anatokea TAKUKURU lakini pia ni mwakilishi wa Chama cha Mawakili wa Serikali akichangia katika mjadala wa kuboresha Daftari la Orodha ya Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria leo tarehe 16/07/2024.
Baadhi ya wadau wa kikao cha kuboresha Daftari la Orodha ya Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria wakifuatilia wasilisho la rasimu ya daftari la orodha ya watoa huduma wa Msaada wa kisheria leo tarehe 16/07/2024 Mtumba Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo akizungumza katika kikao cha ufunguzi wa kazi ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali za Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka 2023/2024, katika ukumbi wa Wizara Mtumba jijini Dodoma, Julai 15, 2024.