Kwa changamoto yoyote ya Kisheria wasiliana nasi kupitia Kituo cha Huduma kwa Mteja.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Ndg. Adolf Ndunguru, (mgeni rasmi) akihitimisha rasmi mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria kuhusu Huduma za Msaada wa Kisheria, tarehe 30 Januari, 2026, Lush Garden jijini Arusha.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Chacha Maswi, akizungumza na washiriki wakati wa hafla ya ufungaji rasmi mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria, tarehe 30 Januari, 2026, Lush Garden jijini Arusha.
Mkurugenzi, Idara ya Huduma za Msaada wa Kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Ester Msambazi, akizungumza na washiriki wakati wa hafla ya ufungaji rasmi mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria, tarehe 30 Januari, 2026, Lush Garden jijini Arusha.
Mkurugenzi, Idara ya Huduma za Sheria Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Ndg. Richard Odongo akiwasilisha jambo wakati wa hafla ya ufungaji rasmi mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria, tarehe 30 Januari, 2026, Lush Garden jijini Arusha.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Chacha Maswi (kushoto) akitoa kompyuta mpakato(laptop) kwa Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria kutoka Tawala na Mikoa na Serikali za Mitaa, wakati wa kuhitimisha mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria kuhusu Huduma za Msaada wa Kisheria, tarehe 30 Januari, 2026, Lush Garden jijini Arusha.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Zainab Katimba akijibu swali la Mhe. Abubakar Asenga Mbunge wa Kilombero kuhusu jitihada za Serikali upatikanaji wa vyeti vya kuzaliwa katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara tarehe 29 Januari, 2026 Bungeni jijini Dodoma
CPA. Amos Makala, Mkuu wa Mkoa wa Arusha aliyemuwakilisha Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, akizungumza na Mawakili wa serikali na Maafisa Sheria wakati wa ufunguzi rasmi wa mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria, mafunzo haya ya siku tatu yameanza leo na yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 30 Januari, 2026 katika ukumbi wa Lush Garden jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Huduma za Msaada wa Kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Ester Msambazi akiwasilisha mada wakati wa mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria, mafunzo haya ya siku tatu yameanza leo na yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 30 Januari, 2026 katika ukumbi wa Lush Garden jijini Arusha.
Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria wakiwa katika mafunzo ya kujengeana uelewa kuhusu masuala ya Huduma za Msaada wa Kisheria, mafunzo haya yaliyoanza leo yanafanyika kwa siku tatu tarehe 28-30 Januari, 2026 katika ukumbi wa Lush Garden Jijini Arusha.