Mkurugenzi wa Katiba na Ufuatiliaji Haki kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Jane Lymo (kushoto) akimuelezea Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera (kulia) namna Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Wizara kinavyofanya kazi katika kuwahudumia wananchi, wakati ambapo waziri alitembelea kituo hicho, 5 Februari, 2026, Mtumba jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Gabriel Omar, akimuelezea Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera (hayupo pichani), namna Mifumo ya TEHAMA ya Wizara inavyotoa huduma za kisheria kwa wananchi, 5 Februari, 2026 Mtumba, jijini Dodoma
Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Mhe. Jaji Winifrida Korosso (Katikati) katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Ndg, Eliakim Maswi (kulia) na Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria Ndg. George Mandepo (kushoto) pamoja na viongozi wengine baada ya kikao cha kujadili nchango wa sekta ya Sheria katika kuwezesha na kufikia malengo ya Dira 2050, tarehe 6 Februari, 2026, Mtumba Jijini Dodoma
Kwa changamoto yoyote ya Kisheria wasiliana nasi kupitia Kituo cha Huduma kwa Mteja.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Ndg. Adolf Ndunguru, (mgeni rasmi) akihitimisha rasmi mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria kuhusu Huduma za Msaada wa Kisheria, tarehe 30 Januari, 2026, Lush Garden jijini Arusha.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Chacha Maswi, akizungumza na washiriki wakati wa hafla ya ufungaji rasmi mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria, tarehe 30 Januari, 2026, Lush Garden jijini Arusha.
Mkurugenzi, Idara ya Huduma za Msaada wa Kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Ester Msambazi, akizungumza na washiriki wakati wa hafla ya ufungaji rasmi mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria, tarehe 30 Januari, 2026, Lush Garden jijini Arusha.
Mkurugenzi, Idara ya Huduma za Sheria Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Ndg. Richard Odongo akiwasilisha jambo wakati wa hafla ya ufungaji rasmi mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria, tarehe 30 Januari, 2026, Lush Garden jijini Arusha.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Chacha Maswi (kushoto) akitoa kompyuta mpakato(laptop) kwa Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria kutoka Tawala na Mikoa na Serikali za Mitaa, wakati wa kuhitimisha mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria kuhusu Huduma za Msaada wa Kisheria, tarehe 30 Januari, 2026, Lush Garden jijini Arusha.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Zainab Katimba akijibu swali la Mhe. Abubakar Asenga Mbunge wa Kilombero kuhusu jitihada za Serikali upatikanaji wa vyeti vya kuzaliwa katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara tarehe 29 Januari, 2026 Bungeni jijini Dodoma