Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Marry Makondo (kulia) kwenye picha ya pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali baada ya kikao cha kutia saini kuingia makubaliano ya kuunda Mfumo wa Uwajibikaji wa Sekta mbalimbali (Multisectoral Accountability Framework - MAF) tarehe 21 Machi, 2023 Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Philipo Gekul (katikati) katika picha ya Pamoja na baadhi ya watumishi na Menejimenti ya RITA, tarehe 17 Machi, 2023 Jijini Dar es Salaam.
Kabidhi Wasii Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) Bi. Angela Anatory (kulia) akitoa taarifa ya utendaji kwa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Philipo Gekul (kushoto) aliyefanya ziara katika ofisi za RITA tarehe 17 Machi, 2023 Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Bw. Leonard Magacha (kulia) akimwonesha Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Florent Kyombo (Mb) na Wajumbe wa Kamati hiyo alioambatana nao kwenye ukaguzi wa ukarabati wa jengo la Mahakama lililokuwa likitumika kama Ofisi ya Serikali za Mitaa. Tarehe 14 Machi, 2023 mjini Tabora.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro katika picha ya pamoja na Dkt. Ines Kajiru na timu yake tarehe 13 Machi, 2023 ofisi za Wizara ya Katiba na Sheria Mtumba Jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro katika mazungumzo na Dkt. Ines Kajiru pamoja na timu yake tarehe 13 Machi, 2023 katika ofisi za Wizara ya Katiba na Sheria Mtumba Jijini Dodoma.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia mazungumzo wakati wa kikao cha Wizara ya Katiba na Sheria na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria. Tarehe 12 Machi, 2023 Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo (mbele kushoto) akiandika maelekezo yaliyokuwa yakitolewa na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria. Tarehe 12 Machi, 2023 Jijini Dodoma.
Watumishi wanawake wa Wizara ya Katiba na Sheria wakati wa maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa katika Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma, tarehe 08 Machi, 2023.
Mhe. Dkt. Damas Daniel Ndumbaro, Waziri wa Katiba na Sheria katika picha ya pamoja na wajumbe wa Menejimenti ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto pamoja na watumishi wa chou hicho tarehe 06 Machi, 2023.