Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera (wa kwanza kulia) akitoa huduma kwa mwananchi aliyetembelea banda la wizara wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam, 3 Julai, 2026, wa pili kushoto ni Katibu Mkuu, Dkt. Seif Shekalaghe.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera (wa kwanza kulia) pamoja na Katibu Mkuu, Dkt. Seif Shekalaghe (wa pili kulia) wakipata maelezo kutoka kwa Wakili wa Serikali, Bw. Herman Mpogole walipotembelea banda la wizara wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam, 3 Julai, 2026.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Katimba (wa pili kulia) akitoa huduma kwa wananchi waliofika kupata huduma katika banda la wizara, wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara yanayofanyika katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam, 1 Julai, 2026.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Katimba (katikati), katika picha ya pamoja na baadhi ya wakurugenzi na watumishi wa wizara, baada ya kutembelea banda la wizara na kutoa huduma kwa wananchi waliofika kupata huduma, wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara yanayofanyika katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam, 1 Julai, 2026.
Baadhi ya wananchi waliotembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria, wakipata huduma kutoka kwa wataalam wa wizara, ikiwa ni sehemu ya ushiriki wa wizara katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja Sabasaba jijini Dar es Salaam, 30 Juni, 2026.
Baadhi ya wananchi waliotembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria, wakipata huduma kutoka kwa wataalam wa wizara, ikiwa ni sehemu ya ushiriki wa wizara katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja Sabasaba jijini Dar es Salaam, 30 Juni, 2026.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Katimba, amefika katika Ofisi za Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TANTRADE) zilizopo katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE, Dkt. Latifa Khamis, na baadaye kutembelea baadhi ya mabanda ya taasisi zinazoshiriki Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara, 29 Juni, 2026.
Katibu Mkuu, Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Abdallah Shekalaghe, akisaini kitabu cha wageni baada ya kuripoti rasmi katika Makao Makuu ya Wizara yaliyopo Mtumba, jijini Dodoma, 29 Juni, 2026.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Haki za Binadamu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Beatrice Mpembo, akitoa elimu ya sheria kwa wananchi waliotembelea banda la wizara wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara, yanayofanyika katika viwanja vya Sabasaba, jijini Dar es Salaam, 29 Juni, 2026.
Wananchi mbalimbali wakiendelea kupata huduma za kisheria kutoka kwa wataalam wa Wizara ya Katiba na Sheria, walipotembelea banda la wizara wakati wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam, 29 Juni, 2026.