Siku ya Mazingira Duniani tarehe 05 Juni, 2026
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. John Jingu, akiwa pamoja na Kamishna Jenerali wa Magereza, Jeremia Katundu mara baada ya kukamilika kwa kikao cha majadiliano ya kuimarisha ushirikiano katika utoaji wa huduma za Msaada wa Kisheria Magerezani.Mazungumzo hayo yalifanyika tarehe 03 Juni, 2026 Mtumba jijini Dodoma
Mkurugenzi wa Katiba na Ufuatiliaji Haki Jane Lyimo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Wataalamu kutoka Taasisi za mnyororo wa Haki Jinai kujadili maendeleo ya Mfumo wa National Legal Information System (NALIS).Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Wizara Mtumba Jijini Dodoma, tarehe 03 Juni, 2026
Mkurugenzi wa Haki za Binadamu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Nkasori Sarakikya akimwakilisha Waziri wa Katiba na Sheria wakati wa uzinduzi wa Bustani ya Miti iliyoanzishwaa mwaka 2022 Nkuhungu jijini Dodoma, kwa lengo la kuimarisha uhifadhi wa mazingira,kukuza ustawi wa jamii na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Zainab Katimba (Kushoto) akikabidhi tuzo ya Shukran kwa Naibu Katibu Mkuu Dkt. Franklin Rwezimula kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. John Jingu kwa kutambua mchango wake katika kufanikisha Mbio za Wakili Marathon zilizofanyika Mei 31, 2026 Jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera (Katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mkakati wa Kitaifa wa Haki Mwanamke Mei 21, 2026 Jijini Dodoma
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Zainab Katimba akijibu swali la Mbunge wa Tunduru ,Mhe. Ado Shaibu, kuhusu mpango wa Serikali wa kutekeleza mapendekezo yaliyotolewa na Tume ya Haki Jinai Bungeni, Jijini Dodoma
Naibu Waziri wa Katiba Sheria Mhe. Zainab Katimba (Wa tatu kulia) akiwa ameambatana na Naibu Katibu Mkuu Dkt. Franklin Rwezimula (Wa pili Kulia) wakiwa katika mbio za Wakili Marathon zilizofanyika Mei 31, 2026 jijini Dodoma zikiwa na lengo la kukusanya fedha zitakazosaidia kutoa huduma za Msaada wa Kisheria kwa Wananchi wasio na uwezo wa kugharamia huduma hiyo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufani mara baada ya kukamilika kwa hafla ya uapisho wa Majaji hao iliyofanyika Ikulu Jijini, Dar es Salaam tarehe 26 Mei, 2026
Timu ya Wataalam wa Wizara ya Katiba na Sheria na wadau kutoka katika Taasisi za Serikali wakiwa katika kikao cha pamoja na timu ya Shirikisho la Urusi kwa ajili ya kupitia mikataba mitatu ya ushirikiano kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Shirikisho hilo yenye lengo la kuimarisha ushirikiano wa kisheria na mapambano dhidi ya uhalifu wa kimataifa.