Wananchi wa Mkoa wa Njombe, wakiendelea kupata huduma za msaada wa kisheria kutoka kwa wataalam wa sheria, huduma hizi zinatolewa ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Awamu ya Pili, 19 Septemba, 2026, Njombe.
Wananchi wa wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma, wakiendelea kupata huduma za msaada wa kisheria kutoka kwa wataalam wa sheria, huduma hizi zinatolewa ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Awamu ya Pili, 19 Septemba, 2026, Namtumbo.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza na baadhi ya watumishi (hawapo pichani) wanaokwenda kuiwakilisha wizara katika Mashindano ya Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI), 18 Septemba, 2026, Mtumba Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Shekalaghe (kulia), akikabidhi Jezi itakayotumiwa na timu ya Katiba Sports Club wakati wa mashindano ya SHIMIWI, anaepokea jezi kwa niaba ya wachezaji ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Utawala, Bw. Peter Sumbuka Bunyazu, 18 Septemba, 2026, Mtumba, Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Shekalaghe (katikati) katika picha pa pamoja na Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu, Bw. Alfred Dede (wa pili kushoto) pamoja na watumishi wa wizara wanaoenda kushiriki mashindano ya Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) 18 Septemba, 2026, Mtumba 4Dodoma.
Baadhi ya wananchi waliofika katika viwanja vya stendi ya zamani Halmashauri ya Njombe Mji, wakipata huduma za msaada wa kisheria zinazotekelezwa na Wizara ya Katiba na Sheria kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Awamu ya Pili, 18 Septemba, 2026, Njombe.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera (kushoto) akikabidhi magodoro wakati alipotembelea Gereza la Mahabusu Songea kwa lengo la kufanya ufuatiliaji wa hali ya upatikanaji wa haki kwa Wafungwa na Mahabusu, pamoja na kusikiliza na kushughulikia changamoto zinazowakabili 17 Septemba, 2026, Songea Ruvuma.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera (katikati) katika picha ya pamoja na viongozi na watumishi kutoka wizarani na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma wakati alipotembelea Gereza la Mahabusu Songea kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji wa hali ya upatikanaji haki kwa Wafungwa na Mahabusu, pamoja na kusikiliza na kushughulikia changamoto zinazowakabili, 17 Septemba, 2026.
Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Gabriel Omarakifunga rasmi kikao kazi cha Wasajili Wasaidizi wa Mikoa na Wanasheria wa Mikoa kuhusu uendelevu na uimarishaji wa huduma za msaada wa kisheria nchini 17 Septemba, 2026 Morogoro.
Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Gabriel Omar (katikati) katika picha ya pamoja na Wasajili Wasaidizi wa Mikoa na Wanasheria wa Mikoa baada ya kufunga rasmi kikao kazi kuhusu endelevu na uimarishaji wa huduma za msaada wa kisheria nchini 17 Septemba, 2026 Morogoro.