Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Homera akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa utekelezaji wa programu ya Sema na Waziri iliyofanyika kupitia Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Wizara,24 Agosti, 2026, Mtumba, jijini Dodoma
Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Homera (kushoto) akizungumza na wananchi wenye changamoto zinazohitaji utatuzi wa kisheria, waliopiga simu kupitia kituo cha Huduma kwa Mteja cha Wizara, wakati wa programu ya Sema na Waziri, 24 Agosti, 2026, Mtumba, jijini Dodoma.
Una changamoto, maoni ama ushauri kuhusu masuala ya kisheria? zungumza moja kwa moja na Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera, jumatatu hii 24 Agosti 2026 kuanzia saa 04:00 Asubuhi.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, akichangia jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria cha kujadili taarifa ya uendeshaji wa mashauri ya wanawake, watoto na watu wenye ulemavu katika vyombo vya upatikanaji haki nchini Bungeni jijini Dodoma, 18 Agosti, 2026
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Edwin Swale (kushoto), akiongoza kikao cha kujadili taarifa ya uendeshaji wa mashauri ya wanawake, watoto na watu wenye ulemavu katika vyombo vya upatikanaji haki nchini iliyowasilishwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, Bungeni jijini Dodoma, 18 Agosti, 2026.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Abdallah Shekalaghe (katikati) kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka alipotembelea ofisi hiyo, 13 Agosti, 2026 jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Abdallah Shekalaghe (kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka, Bw. Sylvester A. Mwakitalu, alipotembelea Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, 13 Agosti, 2026 jijini Dodoma.
Kwa changamoto yoyote ya kisheria, malalamiko, ushauri ama ufafanuzi wa masuala ya kisheria, tupigie Jumatatu hadi Ijumaa, Saa 1:30 Asubuhi hadi saa 11:00 jioni. Wizara ya Katiba na Sheria ''Haki, Usawa na Utawala wa Sheria kwa wote''
Naibu Waziri Wizara ya Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Athuman Katimba (wa kwanza kulia) akifuatilia kwa makini shughuli za kilele cha Maonesho na Sikukuu ya Wakulima (Nanenane), yaliyofanyika katika viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, 8 Agosti, 2026.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Balozi. Baraka Haran Luvanda (katikati) akimuhudumia mwananchi aliyefika katika banda la wizara wakati wa Maonesho ya Wakulima (Nanenane), yaliyofanyika katika viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, 8 Agosti, 2026.