Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, akifungua rasmi mafunzo maalum kwa Mawakili wa Serikali (hawapo pichani), 18 Mei, 2026, jijini Arusha.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa mafunzo maalum kwa Mawakili wa Serikali (hawapo pichani), 18 Mei, 2026, jijini Arusha.
Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Ally Possi, akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa mafunzo maalum kwa Mawakili wa Serikali (hawapo pichani), 18 Mei, 2026, jijini Arusha.
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Samwel Maneno akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa mafunzo maalum kwa Mawakili wa Serikali (hawapo pichani), 18 Mei, 2026, jijini Arusha.
Mawakili wa Serikali wakiwa katika mafunzo maalumu yaliyolenga kuwajengea uwezo juu ya mbinu za kisasa katika usimamizi wa mashauri ya Serikali, 18 Mei, 2026, jijini Arusha.
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Usuluhishi wa Migogoro kwa Njia Mbadala (Alternative Dispute Resolutions-ADR) kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Felix Chakila, akikabidhi cheti cha mafunzo kwa baadhi ya wajumbe wa Bodi za Usuluhishi wa Ndoa wilaya ya Ngara mkoani Kagera, 14 Mei, 2026.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Julius Mtatiro, ametembelea baadhi ya maeneo inakofanyika Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia-Awamu ya Pili katika Manispaa ya Shinyanga ambapo amepokea maelezo ya utekelezaji kutoka kwa Mratibu wa Kampeni hiyo Mkoa wa Shinyanga, Ndg. Raulent Burilo.
Wananchi wa Mkoa wa Shinyanga wanaendelea kupatiwa huduma za msaada wa kisheria kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Awamu ya Pili inayotekelezwa katika halmashauri zote za mkoa huo bila malipo, kampeni ilianza tarehe 6 Mei, 2026 na inatarajiwa kuhitimishwa tarehe 20 Mei, 2026,
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, akiwasikiliza na kuwahudumia wananchi wakati wa programu ya ''Sema na Waziri'', inayoendeshwa kupitia Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Wizara, 7 Mei, 2026, Mtumba, Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Zainab Athuman Katimba, akijibu swali kuhusu hatua zinazochukuliwa na serikali katika kuimarisha taasisi ya ndoa na kushughulikia migogoro ya kifamilia, wakati wa shughuli za Bunge la Kumi na Tatu, Mkutano wa Tatu, Kikao cha Ishirini na Nne, 07 Mei, 2026, Bungeni, jijini Dodoma.