Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, akichangia jambo wakati wa majadiliano ya Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa mwaka 2026 (The Written Laws Miscellaneous Amendment Bill) Muswada umewasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari (hayupo pichani), kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Bungeni jijini Dodoma, tarehe 3 Machi, 2026.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari, akiwasilisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa mwaka 2026 (The Written Laws Miscellaneous Amendment Bill) kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), Bungeni jijini Dodoma, tarehe 3 Machi, 2026.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) imepokea na kujadili Mswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa mwaka 2026 (The Written Laws Miscellaneous Amendment Bill) uliowasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari, Bungeni Dodoma, 3 Machi, 2026.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Katimba, akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa mwaka wa Mahakama, jijini Arusha, tarehe 2 Februari, 2026.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Zainab Katimba akizungumza na Wananchi waliofika kupata huduma katika Kituo Jumuishi cha Masuala ya Familia Temeke Dar es Salaam tarehe 25 Februari, 2026
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Eliakim Maswi akigawa vitendea kazi vya kisasa kwa baadhi ya watumishi wa wizara ili kuongeza kasi katika kuhudumia wananchi, hafla ya ugawaji wa vifaa ilifanyika katika ofisi za Wizara Mtumba Jijini Dodoma, 23 Februari, 2026.
Kwa changamoto yoyote ya Kisheria tafadhali wasiliana nasi bure kwa namba zinazoonekana hapa.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera akishiriki katika Mkutano wa Ngazi ya Juu ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa unaofanyika Nchini Geneva, Uswisi, tarehe 23-24 Februari, 2026.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Zainab Katimba (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Kikosi Kazi cha Ulinzi wa Mtoto dhidi ya biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu mara baada ya kutembelea ofisi za Kikosi Kazi hicho na kupokea taarifa ya utendaji kazi, leo tarehe 23 Februari, 2026, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Zainab Katimba ametembelea Ofisi inayotumiwa na Kikosi kazi cha Ulinzi wa mtoto dhidi ya biashara haramu ya usafirishaji wa binadam na kukagua miundo mbinu ya kidigitali inayotumiwa na kikosi kazi hicho katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku, tarehe 23 Februari, 2026 Jijini Dar Es Salaam.