Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Maswi (katikati), katika picha ya pamoja na Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), Prof. Charles Kihampa (wa tatu kutoka kulia), Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe anayeshughulikia Taaluma, Utafiti na Ushauri, Prof. Hawa Tundui (wa tatu kutoka kushoto), wahadhiri kutoka kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu Mzumbe,pamoja na Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria baada ya kikaocha kujadili mikakati ya kuboresha sekta ya Sheria nchini, hususan katika ngazi ya vyuo vikuu, tarehe 12 Februari, 2026.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Maswi, akiongoza kikao cha kujadili mikakati ya kuboresha sekta ya Sheria nchini, hususan katika ngazi ya vyuo vikuu, kikao kilihudhuriwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), Prof. Charles Kihampa pamoja na wahadhiri wa kitivo cha Sheria Chuo Kikuu Mzumbe na menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria (hawapo pichani), tarehe 12 Februari,2026, Mtumba jijini Dodoma.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), Prof. Charles Kihampa akichangia jambo wakati wa kikao cha kujadili mikakati ya kuboresha sekta ya Sheria nchini, hususan katika ngazi ya vyuo vikuu, kikao kilifanyika katika ofisi za Wizara ya Katiba na Sheria, tarehe 12 Februari,2026, Mtumba jijini Dodoma.
Kwa changamoto zote za kisheria wasiliana nasi kupitia kituo chetu cha Huduma kwa Mteja
Mkurugenzi wa Katiba na Ufuatiliaji Haki kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Jane Lymo (kushoto) akimuelezea Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera (kulia) namna Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Wizara kinavyofanya kazi katika kuwahudumia wananchi, wakati ambapo waziri alitembelea kituo hicho, 5 Februari, 2026, Mtumba jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Gabriel Omar, akimuelezea Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera (hayupo pichani), namna Mifumo ya TEHAMA ya Wizara inavyotoa huduma za kisheria kwa wananchi, 5 Februari, 2026 Mtumba, jijini Dodoma
Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Mhe. Jaji Winifrida Korosso (Katikati) katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Ndg, Eliakim Maswi (kulia) na Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria Ndg. George Mandepo (kushoto) pamoja na viongozi wengine baada ya kikao cha kujadili nchango wa sekta ya Sheria katika kuwezesha na kufikia malengo ya Dira 2050, tarehe 6 Februari, 2026, Mtumba Jijini Dodoma
Kwa changamoto yoyote ya Kisheria wasiliana nasi kupitia Kituo cha Huduma kwa Mteja.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Ndg. Adolf Ndunguru, (mgeni rasmi) akihitimisha rasmi mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria kuhusu Huduma za Msaada wa Kisheria, tarehe 30 Januari, 2026, Lush Garden jijini Arusha.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Chacha Maswi, akizungumza na washiriki wakati wa hafla ya ufungaji rasmi mafunzo ya Mawakili wa Serikali na Maafisa Sheria, tarehe 30 Januari, 2026, Lush Garden jijini Arusha.