Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera (Mb), akifungua rasmi Kikao cha Nne cha Baraza la Nane la wafanyakazi wa Wizara ya Katiba na Sheria kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, jijini Dodoma, 23 Machi, 2026.
Katibu Mkuu, Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Maswi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la wafanyakazi la Wizara ya Katiba na Sheria, akizungumza jambo, wakati wa Kikao cha Nne cha Baraza la Nane la wafanyakazi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, jijini Dodoma, 23 Machi, 2026.
Baadhi ya Viongozi na watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiimba wimbo wa mshikamano wakati wa Kikao cha Nne cha Baraza la Nane la wafanyakazi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, jijini Dodoma, 23 Machi, 2026.
Baadhi ya viongozi na watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakishiriki Kikao cha Nne cha Baraza la Nane la wafanyakazi, kilichofanyika katika Ukumbi wa TAKWIMU jijini Dodoma, 23 Machi, 2026.
Mawakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba Sheria wakiwasikiliza wananchi waliofika kupata huduma za Msaada wa Kisheria wakati wa ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mkoani Katavi, 17 Machi, 2026
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe.Dkt. Juma Zuberi Homera (wa kwanza kushoto) akiwahudumia wananchi kupitia Kituo cha Huduma Kwa Mteja cha Wizara, mara baada ya kuzindua programu ya Sema na Waziri, 17 Machi, 2026, Mtumba, jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Katimba (wa kwanza kushoto) akiwahudumia wananchi kupitia Kituo cha Huduma Kwa Mteja cha Wizara, mara baada ya uzinduzi wa programu ya Sema na Waziri, iliyozinduliwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera,17 Machi, 2026, Mtumba, jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera (wa pili kushoto-waliosimama msitari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Katimba (wa tatu kushoto) pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakati wa uzinduzi wa programu ya Sema na Waziri kupitia Kituo cha Huduma Kwa Mteja cha Wizara, 17 Machi, 2026, Mtumba, jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Juma Zuberi Homera, akichangia jambo wakati wa uwasilishwaji wa Muswada wa mabadiliko ya Sheria mbalimbali ikiwemo sheria ya Tafsiri ya sheria mbalimbali sura (1) ya mwaka 2026 uliowasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari (hayupo pichani) kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Bungeni, jijini Dodoma, 3 Machi, 2026
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari, akiwasilisha Muswada wa mabadiliko ya Sheria mbalimbali ikiwemo sheria ya Tafsiri ya sheria mbalimbali sura (1) ya mwaka 2026 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Bungeni, jijini Dodoma, 3 Machi, 2026.