Mkurugenzi Kitengo cha Utajiri Asili na Maliasilia za Nchi kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, DCP. Neema Mwanga, (wa kwanza kushoto) akimsikiliza mwananchi aliyetembelea banda la wizara kwa ajili ya kupata huduma za msaada wa kisheria wakati wa Maonesho ya Wakulima yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, 5 Agosti, 2026.
Wizara ya Katiba na Sheria inashiriki katika Maonesho ya Wakulima (NaneNane) yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma ambapo elimu ya na huduma nyingine za kisheria zinatolewa kwa wananchi wa rika zote.
Wakili wa Serikali akimsikiliza mwananchi aliyefika katika banda la Wizara ya Katiba na Sheria kwenye Maonesho ya Wakulima NaneNane jijini Dodoma kwa ajili ya kupata huduma za kisheria
Karibuni katika Maonesho ya Wakulima NaneNane jijini Dodoma kwa huduma na elimu kuhusu masuala ya Kisheria.
Wananchi wakipata huduma za msaada wa kisheria na elimu ya kisheria kati banda la wizara ya Katiba na Sheria kwenye Maonesho ya Wakulima NaneNane jijini Dodoma.
Wizara imeendelea kutumia redio za kijamii katika kuhakikisha elimu kuhusu upatikanaji wa huduma za kisheria zinawafikia wananchi katika Mikoa mbalimbali Nchini. Wakili wa Serikali Erick Salila akitoa elimu kupitia Redio Baraka FM iliyopo Mkoani Mbeya
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Balozi. Baraka Luvanda, akisaini kitabu wakati aliporipoti rasmi tarehe 24 Julai, 2026 Wizarani Mtumba jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza na Menejimenti ya wizara (hawapo pichani) katika kikao kilichofanyika katika ofisi za wizara Mtumba, jijini Dodoma, 21 Julai, 2026.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Shekalaghe (kulia) akipokea kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria Tuzo ya Mshindi wa kwanza katika kundi la wizara zilizoshiriki Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara yaliyofanyika jijini Dar es salaam, kuanzia tarehe 28 Juni hadi 13 Julai, 2026, anayekabidhi tuzo ni Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Bi. Hyasinta Kissima, 21 Julai, 2026.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Shekalaghe (kulia) akipokea Tuzo ya Utambuzi, iliyotolewa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Utajiri Asilia na Mali asili za Nchi, DCP. Neema Mwanga 21 Julai, 2026, Mtumba jijini Dodoma.