Naibu Waziri Wizara ya Katiba na Sheria, Mhe. Zainab Athuman Katimba (wa kwanza kulia) akifuatilia kwa makini shughuli za kilele cha Maonesho na Sikukuu ya Wakulima (Nanenane), yaliyofanyika katika viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, 8 Agosti, 2026.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Balozi. Baraka Haran Luvanda (katikati) akimuhudumia mwananchi aliyefika katika banda la wizara wakati wa Maonesho ya Wakulima (Nanenane), yaliyofanyika katika viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, 8 Agosti, 2026.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Balozi. Baraka Haran Luvanda (katikati) katika picha ya pamoja na wakurugenzi na watumishi wa wizara wakati wa kilele cha Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane), yaliyofanyika katika viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, 8 Agosti, 2026.
Mkurugenzi Kitengo cha Utajiri Asili na Maliasilia za Nchi kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, DCP. Neema Mwanga, (wa kwanza kushoto) akimsikiliza mwananchi aliyetembelea banda la wizara kwa ajili ya kupata huduma za msaada wa kisheria wakati wa Maonesho ya Wakulima yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma, 5 Agosti, 2026.
Wizara ya Katiba na Sheria inashiriki katika Maonesho ya Wakulima (NaneNane) yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma ambapo elimu ya na huduma nyingine za kisheria zinatolewa kwa wananchi wa rika zote.
Wakili wa Serikali akimsikiliza mwananchi aliyefika katika banda la Wizara ya Katiba na Sheria kwenye Maonesho ya Wakulima NaneNane jijini Dodoma kwa ajili ya kupata huduma za kisheria
Karibuni katika Maonesho ya Wakulima NaneNane jijini Dodoma kwa huduma na elimu kuhusu masuala ya Kisheria.
Wananchi wakipata huduma za msaada wa kisheria na elimu ya kisheria kati banda la wizara ya Katiba na Sheria kwenye Maonesho ya Wakulima NaneNane jijini Dodoma.
Wizara imeendelea kutumia redio za kijamii katika kuhakikisha elimu kuhusu upatikanaji wa huduma za kisheria zinawafikia wananchi katika Mikoa mbalimbali Nchini. Wakili wa Serikali Erick Salila akitoa elimu kupitia Redio Baraka FM iliyopo Mkoani Mbeya
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Balozi. Baraka Luvanda, akisaini kitabu wakati aliporipoti rasmi tarehe 24 Julai, 2026 Wizarani Mtumba jijini Dodoma.