Baadhi ya wananchi waliofika katika viwanja vya stendi ya zamani Halmashauri ya Njombe Mji, wakipata huduma za msaada wa kisheria zinazotekelezwa na Wizara ya Katiba na Sheria kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Awamu ya Pili, 18 Septemba, 2026, Njombe.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera (kushoto) akikabidhi magodoro wakati alipotembelea Gereza la Mahabusu Songea kwa lengo la kufanya ufuatiliaji wa hali ya upatikanaji wa haki kwa Wafungwa na Mahabusu, pamoja na kusikiliza na kushughulikia changamoto zinazowakabili 17 Septemba, 2026, Songea Ruvuma.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera (katikati) katika picha ya pamoja na viongozi na watumishi kutoka wizarani na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma wakati alipotembelea Gereza la Mahabusu Songea kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji wa hali ya upatikanaji haki kwa Wafungwa na Mahabusu, pamoja na kusikiliza na kushughulikia changamoto zinazowakabili, 17 Septemba, 2026.
Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Gabriel Omarakifunga rasmi kikao kazi cha Wasajili Wasaidizi wa Mikoa na Wanasheria wa Mikoa kuhusu uendelevu na uimarishaji wa huduma za msaada wa kisheria nchini 17 Septemba, 2026 Morogoro.
Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Gabriel Omar (katikati) katika picha ya pamoja na Wasajili Wasaidizi wa Mikoa na Wanasheria wa Mikoa baada ya kufunga rasmi kikao kazi kuhusu endelevu na uimarishaji wa huduma za msaada wa kisheria nchini 17 Septemba, 2026 Morogoro.
Mkurugenzi Msaidizi wa Uratibu wa Huduma za Msaada wa Kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Lucy Diganyeck, akifungua rasmi Kikao Kazi cha Wasajili Wasaidizi na Wanasheria wa Mikoa kuhusu uendelevu na uimarishaji wa huduma za msaada wa kisheria nchini 16 Septemba, 2026 Morogoro.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Balozi. Baraka Luvanda, akifungua rasmi kikao cha wadau katika Mnyororo wa Haki Jinai kilichofanyika kwa lengo la kupitia na kuiboresha Rasimu ya Mwongozo wa Ufuatiliaji wa Majukumu ya Taasisi za Haki Jinai, 15 Septemba, 2026, Mtumba, jijini Dodoma.
Baadhi ya wadau katika mnyororo wa Haki Jinai wakiwa katika kikao cha kupitia na kuiboresha Rasimu ya Mwongozo wa Ufuatiliaji wa Majukumu ya Taasisi za Haki Jinai, 15 Septemba, 2026, Mtumba jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Katiba na Sheria, Balozi. Baraka Luvanda (katikati) katika picha ya pamoja na wadau katika mnyororo wa Haki Jinai baada ya kikao cha kupitia na kuiboresha Rasimu ya Mwongozo wa Ufuatiliaji wa Majukumu ya Taasisi za Haki Jinai, 15 Septemba, 2026, Mtumba jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Balozi Baraka Luvanda (wa pili kulia) akiongoza kikao cha ujumbe kutoka Serikali ya Japan kujadili maeneo ya ushirikiano katika sekta ya sheria kati ya Tanzania na Japan.Ujumbe wa Serikali ya Japan ulioongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Pili ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Japan, Bw. Hironori Suzuki (hayupo pichani), akifuatana na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Yoichi Mikami kikao kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma, 15 Septemba, 2026.