Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Balozi. Baraka Luvanda, akifungua rasmi kikao cha wadau katika Mnyororo wa Haki Jinai kilichofanyika kwa lengo la kupitia na kuiboresha Rasimu ya Mwongozo wa Ufuatiliaji wa Majukumu ya Taasisi za Haki Jinai, 15 Septemba, 2026, Mtumba, jijini Dodoma.
Baadhi ya wadau katika mnyororo wa Haki Jinai wakiwa katika kikao cha kupitia na kuiboresha Rasimu ya Mwongozo wa Ufuatiliaji wa Majukumu ya Taasisi za Haki Jinai, 15 Septemba, 2026, Mtumba jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Katiba na Sheria, Balozi. Baraka Luvanda (katikati) katika picha ya pamoja na wadau katika mnyororo wa Haki Jinai baada ya kikao cha kupitia na kuiboresha Rasimu ya Mwongozo wa Ufuatiliaji wa Majukumu ya Taasisi za Haki Jinai, 15 Septemba, 2026, Mtumba jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Balozi Baraka Luvanda (wa pili kulia) akiongoza kikao cha ujumbe kutoka Serikali ya Japan kujadili maeneo ya ushirikiano katika sekta ya sheria kati ya Tanzania na Japan.Ujumbe wa Serikali ya Japan ulioongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Pili ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Japan, Bw. Hironori Suzuki (hayupo pichani), akifuatana na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Yoichi Mikami kikao kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma, 15 Septemba, 2026.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Balozi Baraka Luvanda akiongoza kikao cha ujumbe kutoka Serikali ya Japan kujadili maeneo ya ushirikiano katika sekta ya sheria kati ya Tanzania na Japan.Ujumbe wa Serikali ya Japan ulioongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Pili ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Japan, Bw. Hironori Suzuki (hayupo pichani), akifuatana na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Yoichi Mikami kikao kilichofanyika Mtumba jijini Dodoma, 15 Septemba, 2026.
Mkurugenzi wa Utatuzi wa Migogoro kwa Njia Mbadala kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Felix Chakila, akizungumza jambo wakati wa mazungumzo na ujumbe wa Serikali ya Japan ulioongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Pili ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Japan, Bw. Hironori Suzuki (hayupo pichani), Mtumba jijini Dodoma, 15 Septemba, 2026.
Una Changamoto ya kisheria? malalamiko, maoni ama ushauri? Tupigie Jumatatu hadi Ijumaa saa 1:30 Asubuhi hadi saa 11:00 jioni.
Mkurugenzi Kitengo cha Utajiri Asili na Maliasilia za Nchi, Wizara ya Katiba na Sheria, DCP Neema Mwanga, akitoa zawadi ya kalenda kwa mwananchi aliyetembelea banda la wizara wakati wa Kongamano la 5 la Kimataifa la Uchumi wa Buluu (BEC 2026), katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam, 7 Septemba, 2026.
Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Nickson Maleko (kulia) akitoa elimu kwa mwananchi aliyetembelea banda la wizara wakati wa Kongamano la 5 la Kimataifa la Uchumi wa Buluu (BEC 2026), katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam, 7 Septemba, 2026.
Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Daniel Mbaki (kulia) akitoa elimu kwa mwananchi aliyetembelea banda la wizara wakati wa Kongamano la 5 la Kimataifa la Uchumi wa Buluu (BEC 2026), katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam, 7 Septemba, 2026.