Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akijibu hoja kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, tarehe 18 Machi, 2024 Ofisi za Bunge Dodoma.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama Prof. Elisante Ole Gabriel akisoma Makadirio ya bajeti ya Mahakama kwa mwaka wa fedha 2024/25 mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, tarehe 18 Machi, 2024 Ofisi za Bunge Dodoma.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Mhe. Dkt. Charles Kimei akichangia hoja baada ya Kamati hiyo kupokea Makadirio ya bajeti ya Mahakama kwa mwaka wa fedha 2024/25, tarehe 18 Machi, 2024 Ofisi za Bunge Dodoma.
Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (kulia) akisoma taarifa wakati wa Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, tarehe 18 Machi, 2024 Ofisi za Bunge Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akiongea wakati akitoa shukrani zake kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, tarehe 13 Machi, 2024 ilipotembelea Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Dodoma.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, wakifuatilia wasilisho la mfumo wa Kunukuu na Kutafsiri mwenendo wa mashauri ya Mahakama, tarehe 13 Machi, 2024, walipotembelea Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Dodoma.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kwenye picha ya pamoja na Waziri Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana na Mtendaji Mkuu wa Mahakama Prof. Elisante Ole Gabriel, tarehe 13 Machi, 2024, walipotembelea Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akizungumza na Wanahabari wakati wa ukaguzi uliofanywa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwenye Mradi wa ujenzi wa IJC mkoani Njombe. Tareh 13 Machi, 2024.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Joseph Kizito Mhagama (wa pili kulia) akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa ukaguzi wa Mradi wa Ujenzi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) mkoani Njombe tarehe 13 Machi, 2024.
Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakichangia wasilisho la taarifa ya Mradi wa Ujenzi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki kinachojengwa mkoani Njombe na Mahakama ya Tanzania. Tarehe 13 Machi, 2024.