Watendaji wa Jiji la Tanga wakiwa katika picha ya pamoja na wawezeshaji kutoka Wizara ya Katiba na Sheria mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya Uraia na Utawala Bora yaliyofanyika tarehe 15 Machi, 2025.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda, akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Usalama Mkoa, Wawezeshaji wa Mafunzo ya Utawala Bora na Urai mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya Uraia na Utawala Bora mafunzo yanayoratibiwa na Wizara ya Katiba na Sheria kupitia Idara ya Katiba na Ufuatiliaji Haki. Tarehe 13 Machi, 2025.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Eliakim Maswi alipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Wizara hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma. Tarehe 11 Machi, 2025.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza na wananchi waliofika kupata Huduma za Msaada wa Kisheria wakati alipowasili mapema Machi 4, 2025 Jijini Arusha kwa ajili ya kushiriki katika kutoa Huduma hiyo kuelekea kwenye Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake itakayoadhimishwa Kitaifa Jijini hapo ambapo. Wizara inatoa Huduma za Msaada wa Kisheria kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia bila malipo.
Timu ya Msaada wa Kisheria Jijini Mbeya Machi 2, 2025 imeendelea kutoa elimu ya Msaada wa Kisheria katika nyumba za Ibada.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Jumanne Sagini akizungumza na wananchi waliojitokeza kupatiwa huduma ya msaada wa Kisheria kupitia kampeni ya Mama Samia alipotembelea mabanda ya kutoa huduma hiyo Jijini Arusha, ambapo Wizara inaendelea na zoezi hilo kuelekea Maadhimisho ya siku ya Wanawake. Tarehe 02 Machi, 2025.
Naibu Kamishna wa Polisi DCP Neema Mwanga akizungumza na Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka Nchi ya Japan ambao wametembelea katika Banda la Wizara ya Katiba na Sheria Kabwe jijini Mbeya kwa ajili ya kujifunza kuhusu utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria "Mama Samia Legal Aid " inavyotolewa kwa Wananchi. tarehe Machi 02, 2025.
Jopo la wanasheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria wakitoa huduma ya Msaada wa Kisheria kwa wananchi wa Jiji la Arusha waliojitokeza kupatiwa huduma hiyo hivi karibuni. Tarehe 01 Machi, 2025.
Timu ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia katika picha ya pamoja na viongozi wa serikali ya Kijiji cha Mwananyamala na wananchi baada ya kumaliza mgogoro wa ardhi kati ya serikali ya Kijiji hicho na Bw. Mohamed Chinguile baada ya kuchukuliwa ardhi yake kwaajili ya matumizi ya ujenzi wa shule. Baada ya mvutano wa muda mrefu hatimaye kupitia kampeni hiyo ameridhia kufidiwa kwa kupewa eneo mbadala. Tarehe 01 Machi, 2025.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) ameongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano Tanzania kushiriki katika Kikao cha 58 cha Haki za Binadamu kinachofanyika Geneva Nchini Uswisi. 24 Februari, 2025.