Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Maswi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Baraza la 23 la Wafanyakazi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora. Tarehe 05 Februari, 2025.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora mara baada ya Ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume hiyo lililofanyika Jijini Dodoma. Tarehe 05 Februari, 2025.
Wakurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Sekta 9, zinazohusika na Utajiri Asili na Maliasilia za Nchi wamefanya kikao kazi maalum cha kupitia na kuboresha rasimu ya Mkakati wa Taifa wa utekelezaji wa misingi ya Sheria za Uangalizi wa Utajiri Asili na Maliasili za Nchi Sura Namba 449 na 450.Kikao hicho kimefanyika tarehe 3 Februari, 2025 jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro leo Februari 03, 2025 ameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini ambapo Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Maadhimisho hayo yalifanyika katika Uwanja wa Chinangali, Jijini Dodoma.
Wananchi katika Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi wakifuatilia Elimu zinazotolewa Kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia ambayo katika Mkoa huo ulizinduliwa tarehe 24 Januari, 2025 na inatarajiwa kumalizia tarehe 2, Februari 2025.
Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Fredrick Makamba akizungumza na kutoa Elimu kwa Wananchi kuhusu masuala ya Ardhi, Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi mnamo tarehe 31 Januari, 2025. Timu ya Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (MSLAC), inaendelea na utoaji wa Msaada wa Kisheria kwa Makundi mbalimbali ambapo mpaka sasa Mikoa 17 imefikiwa na Kampeni hiyo.
Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Daniel Mbaki akizungumza na Mzee ambaye ni Mkazi wa Kilimanjaro aliyefika katika banda la Wizara ya Katiba na Sheria kwa ajili ya kupata ufafanuzi kuhusu masuala ya mirathi. Timu ya Wataalamu wa Sheria ipo katika Halmashauri zote za Mkoa wa Kilimanjaro kwa muda wa siku tisa kwa ajili ya kutoa Msaada wa Kisheria bila malipo kupitia Mama Samia Legal Aid Campaign. Tarehe 29 Januari, 2025.
Baadhi ya Wananchi katika Mkoa wa Kilimanjaro wakipata Huduma za Msaada wa Kisheria bila Malipo kupitia Mama Samia Legal Aid Campaign. Mkoa wa Kilimanjaro ulizindua rasmi Kampeni hiyo ulifanyika tarehe 29 Januari, 2025 na inatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku tisa katika Halmashauri zote za Mkoa huo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu, tarehe 27 Januari, 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Timu ya Utangulizi kutoka Wizara ya Katiba na Sheria ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Msaada wa Kisheria Bi. Ester Msambazi (wa kwanza kushoto) ikiwa ni sehemu ya mpango wa Maandalizi ya Utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria Mama Samia Legal Aid Campaign Mkoani Kilimanjaro, mnamo tarehe 29 Januari, 2025.
Mkuu wa Dawati la Kijinsia na Afisa Ustawi Madam Christina akitoa utatuzi wa masuala mbambali kwa wananchi waliofika kusikilizwa katika Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia. Tarehe 26 Januari, 2025 Katavi.