Baadhi ya watumishi wakifuatilia mafunzo elekezi kwa watumishi 73 wa Wizara ya Katiba na Sheria na Tume ya Haki za Binadamu, mafunzo hayo ni ya siku tatu ambayo yanafanyika katika chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere mjini Kibaha.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu kutoka Tume ya Haki za Binadamu Jakson Elias Nyamwiula pamoja na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Fatma Kalovya wakifuatilia mafunzo elekezi kwa watumishi 73 wa Wizara ya Katiba na Sheria na Tume ya Haki za Binadamu..
Watoto wakifurahia elimu kuhusu masuala mbalimbali katika banda la Wizara ya Katiba na Sheria wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Kibiashara Sabasaba 2025.
Wananchi wakiendelea kupata huduma mbalimbali katika banda la Wizara ya Katiba na Sheria wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Kibiashara Sabasaba,
TUPO SABASABA KARIBU TUKUHUDUMIE - "Maonesho ya Kimataifa ya Kibiashara Sabasaba, Fahari ya Tanzania"
TUPO SABASABA KARIBU TUKUHUDUMIE - "Maonesho ya Kimataifa ya Kibiashara Sabasaba, Fahari ya Tanzania"
Wananchi na watumishi wakiendelea kupata huduma mbalimbali katika banda la Wizara ya Katiba na Sheria katika Wiki ya Utumishi wa Umma.
Mkurugenzi Msaidizi Huduma za Kisheria kwa Umma Bw. Abdulrahman Mshamu akionyesha tuzo ya Wizara ya Katiba na Sheria iliyo tolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa wakati Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akikabidhi Tuzo ya ushiriki wa Wizara ya Katiba na Sheria katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene, ameipongeza Wizara ya Katiba na Sheria kwa utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma jijini Dodoma.