Baadhi ya Wakurugenzi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakifuatilia taarifa iliyowasilishwa na Waziri mwenye dhamana Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro jijini Dodoma, tarehe 20 Mei, 2025 wakati akielezea Mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita kwa Waandishi wa Habari kwa kipindi cha miaka minne ya Wizara ya Katiba na Sheria.
Waziri wa Katiba na Sheria akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dodoma Mei 20, 2025 kuelezea Mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita kwa kipindi cha miaka minne ya Wizara ya Katiba na Sheria
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Ismail Ali Ussi (kushoto) akipokea maelezo ya utoaji wa Huduma za Msaada na Elimu ya masuala ya Sheria kwa Wananchi kutoka kwa Wakili wa Serikali George Onyango wa Wizara ya Katiba na Sheria. Kiongozi huyo alitembelea banda la Wizara lililokuwepo kwenye uwanja wa mkesha wa Mwenge Manispaa ya Songea, Mkoani Ruvuma tarehe 5 Mei, 2025.
Washiriki wa kikao kazi cha kupitia rasimu ya Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Haki Jinai wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Franklin Jasson Rwezimula (aliyekaa katikati) baada ya ufunguzi rasmi wa kikao hicho Mei 14, 2025 jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Eliakim Maswi akitoa elimu kuhusu masuala ya ukatili kwa watoto kwenye Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Kusini Unguja, kwa wanafunzi ambao ni wanakikundi cha Sanaa cha Taifa kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba walipotembelea banda la Wizara katika viwanja vya Mtende tarehe 10 Mei, 2025
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) amesema Elimu ya masuala ya kisheria ni msingi wa amani, maendeleo endelevu na mshikamano katika jamii. Dkt. Ndumbaro aliyasema hayo Mei 13, 2025 kwa wananchi wa Manispaa ya Songea (hawapo pichani) wakati akitoa elimu kuhusu masuala ya utawala bora na namna ya kutatua migogoro kwa njia ya kisheria.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kuzindua Kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia, uzinduzi huo uliyofanyika tarehe 10-5-2025 katika viwanja vya Mtende Mkoa wa Kusini Unguja
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akipata maelezo kutoka kwa Wakili wa Serikali Wizara ya Katiba na Sheria Tanzania –URT. Edith Shekidele, wakati akitembelea maonesho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Mtende Mkoa wa Kusini Unguja, kabla ya kuzindua Kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia, uliofanyika 10-5-2025 (kushoto kwa Rais) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Mhe.Haroun Ali Suleiman.
Wananchi mbalimbali waliojitokeza katika uwanja wa Azimio Mtende wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia mkoani Kusini Unguja ambapo mgeni rasmi ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi tarehe 10 Mei, 2025
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi pamoja na viongozi wengine wakiimba wimbo wa taifa wa Zanzibar, Wimbo wa taifa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika uwanja wa Azimio Mtende wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia mkoani Kusini Unguja tarehe 10 Mei 2025