Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Katiba na Sheria

Majukumu ya Wizara

  1. Kuweka Sera kwa ajili ya mambo ya kisheria na utekelezaji wake;
  2. Kushughulikia mambo ya Kikatiba;
  3. Kusimamia mfumo wa haki na utoaji haki;
  4. Kuandika Sheria;
  5. Kuendesha mashtaka ya jinai;
  6. Kuhakiki mikataba mbalimbali inayohusu Serikali,
  7. Kuendeshaji mashauri ya madai yanayohusu Serikali na uratibu wa sheria za kimataifa;
  8. Kushughulikia masuala ya haki za binadamu na msaada wa kisheria;
  9. Kurekebisha sheria mbalimbali za nchi;
  10. Kushughulikia urejeshwaji wa wahalifu na ushirikiano wa mataifa kwenye makosa ya jinai;
  11. Kusajili matukio muhimu ya binadamu kama vizazi, vifo, ndoa, talaka, ufilisi nk;
  12. Kuboresha utendaji na maendeleo ya rasilimali watu iliyo chini ya Wizara;
  13. Kuratibu shughuli za taasisi, mipango na miradi chini ya Wizara.