Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Katiba na Sheria

Majukumu ya Wizara

1. Kushughulikia masuala ya Kikatiba;
2. Kutunga Sera zinazohusu masuala ya kisheria na kusimamia utekelezaji wake;
3. Uandishi wa Sheria;
4. Kusimamia mfumo wa haki na utoaji haki;
5. Kuendesha mashtaka ya jinai;
6. Kushughulikia uendeshaji wa mashauri ya madai na usuluhishi;
7. Usuluhishi wa migogoro ya kibiashara, Sheria za kimataifa na Mikataba;
8. Kuratibu masuala ya haki za binadamu na utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria;
9. Kuratibu usajili wa matukio muhimu ya binadamu, ufilisi na udhamini;
10. Kuratibu tathmini na maboresho ya Sheria;
11. Kuratibu ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa Sheria za Utajiri na Maliasilia za nchi;
12. Kushughulikia urejeshwaji wa wahalifu na masuala ya ushirikiano wa kimataifa kwenye makosa ya jinai;
13. Kuboresha utendaji na maendeleo ya rasilimali watu iliyo chini ya Wizara; na
14. Kuratibu majukumu ya taasisi, mipango na miradi chini ya Wizara