Majukumu ya Wizara
Kwa mujibu wa Hati Idhini ambayo ilitolewa katika Gazeti la Serikali Na. 686 la tarehe 19 Desemba, 2025, Wizara ya Katiba na Sheria ilipewa usimamizi na uratibu wa majukumu yafuatayo: -
1. Kutunga sera zinazohusu masuala ya sheria na kusimamia utekelezaji wake;
2. Kushughulikia masuala ya kikatiba;
3. Kusimamia mfumo wa haki na utoaji haki;
4. Uandishi wa Sheria;
5. Kuendesha mashtaka ya jinai;
6. Kushughulikia uendeshaji wa mashauri ya madai na usuluhishi;
7.Usuluhishi wa migogoro ya kibiashara, Sheria za kimataifa na Mikataba;
8. Kuratibu masuala ya haki za binadamu na utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria;
9. Kusimamia shughuli za ufilisi na udhamini;
10. Kuratibu tathmini na maboresho ya Sheria;
11. Kuratibu ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa Sheria za Utajiri na Maliasilia za nchi;
12. Kushughulikia urejeshwaji wa wahalifu na masuala ya ushirikiano wa kimataifa kwenye makosa ya jinai;
13. Kuboresha utendaji na maendeleo ya rasilimali watu iliyo chini ya Wizara; na
14. Kuratibu majukumu ya taasisi, mipango na miradi chini ya Wizara