Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Katiba na Sheria

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Malengo:

Kutoa huduma na utaalamu katika habari, mawasiliano na mazungumzo na umma na vyombo vya Habari.

kitengo hiki kitatekeleza shughuli zifuatazo:

  1. kuzalisha na kusambaza nyaraka kama vile vipeperushi, makala, jarida la kuhabarisha umma kuhusu sera, programu, shughuli na maboresho yanayofanywa na wizara.
  2. Kuratibu mikutano ya Wizara na waandishi wa Habari.
  3. kushiriki katika majadiliano na umma pamoja na vyombo vya habari kuhusu masuala yanayohusu wizara.
  4. Kukuza, sera, programu na shughuli za Wizara.
  5. kuratibu utayarishaji wa nyaraka za wizara kwa ajili ya warsha na makongamano.
  6. kuratibu utayarishaji na utengenezaji wa makala za wizara na magazeti.
  7. Kuhuisha taarifa za Wizara katika tovuti.
  8. Kushauri Idara, vitengo na taasisi za umma juu ya utengenezaji wa nyaraka mbalimbali.

Hiki kitengo kinaongozwa na Mkuu wa Kitengo ambaye ni Afisa Habari Mkuu