Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt Damas Ndumbaro akizungumza na Maafisa Sheria wa Jeshi la Magereza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa hao kuhusu Huduma za Msaada wa Kisheria, Mapokezi ya wafungwa Magerezani na adhabu mbadala.Mafunzo hayo yalifunguliwa tarehe 5, 2025 mjini Morogoro
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg, Eliakim Maswi akizungumza na Maafisa Sheria wa Jeshi la Magereza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa hao kuhusu Huduma za Msaada wa Kisheria, Mapokezi ya wafungwa Magerezani na adhabu mbadala.Mafunzo hayo yalifunguliwa tarehe 5, 2025 mjini Morogoro
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg, Eliakim Maswi akizungumza na Maafisa Sheria wa Jeshi la Magereza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa hao kuhusu Huduma za Msaada wa Kisheria, Mapokezi ya wafungwa Magerezani na adhabu mbadala.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro (aliyekaa katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Wanasheria wa Jeshi la Magereza mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Maafisa Sheria wa Jeshi la Magereza na Wizara kuhusu Huduma za Msaada wa Kisheria, Mapokezi ya wafungwa Magerezani na adhabu mbadala.Mafunzo hayo yalifunguliwa tarehe 5, 2025 mjini Morogoro
Naibu Waziri Wizara ya Katiba na Sheria (Bara) Mhe. Jumanne Sagini amesema ushirikiano kati ya Wizara upande wa Bara na Zanzibar umewezesha Kampeni ya Msaada wa Kisheria kuwa na mafanikio makubwa. Mhe. Sagini ameyasema hayo leo tarehe 5 Mei, 2025 wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia katika Mkoa wa Kusini Pemba.
Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Khamisi Ramadhani Abdalla akizungumza wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria leo tarehe 5, Mei 2025 Kusini Pemba ambapo amesema Mahakama ya Zanzibar imelenga kukazia njia mbadala ya utatuzi wa migogoro ikiwa ni pamoja na usuluhishi ili kupunguza mrundikano wa kesi mahakamani.
Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Candid Nasua amewaeleza Wanachama wa kikao cha 83 cha Kamisheni ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, kuhusu falsafa ya Rais Samia katika kuhakikisha Haki za Binadamu hazikiukwi ikiwa ni pamoja na Maridhiano, Ustahimilivu ,Mageuzi na Kujenga Upya Taifa ambapo kwa kupitia majadiliano na ushirikiano imechangia katika kuimarisha Haki za Binadamu, umoja wa Kitaifa, Amani pamoja na kuleta maendeleo Nchini. Kikao hicho kinafanyika katika makao makuu ya Kamisheni hiyo jijini Banjul Gambia ambapo Tanzania inawakilishwa na Wizara ya Katiba na Sheria kupitia Idara ya Haki za Binadamu.
Naibu Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa vibali vya ajira kwa sekta ya Mahakama nchini, akishukuru kwa Vibali vya ajira 522 vilivyotolewa mwaka jana na vibali Vingine 1044 vilivyotolewa mwaka huu.Mhe. Sagini aliyasema hayo tarehe 30 Aprili, 2025 wakati akijibu hoja za Wabunge zilizoibuliwa kwenye hotuba ya Bajeti ya Wizara.
Viongozi wa Wizara wakiwa pamoja na Viongozi mbalimbali wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara wakifuatilia uwasilishaji wa Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria bungeni Dodoma 30 Aprili 2025
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akijadiliana jambo na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini wakati wa uwasilishaji wa hotuba ya makadirio ya bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria bungeni Dodoma tarehe 30 Aprili, 2025.