Mkurugenzi Msaidizi Huduma za Kisheria kwa Umma Bw. Abdulrahman Mshamu akionyesha tuzo ya Wizara ya Katiba na Sheria iliyo tolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa wakati Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akikabidhi Tuzo ya ushiriki wa Wizara ya Katiba na Sheria katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene, ameipongeza Wizara ya Katiba na Sheria kwa utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma jijini Dodoma.
Wataalamu wa Wizara ya Katiba na Sheria wakitoa huduma za Masuala ya Utumishi na Utawala, Msaada wa Kisheria, Elimu ya Haki za Binadam pamoja na Elimu ya Uraia na Utawala Bora, Juni 16, 2025 wakati wa maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Franklin Rwezimula (mwenye kofia nyeusi mbele) pamoja na viongozi wengine wakifuatilia Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria kwa Mkoa wa Dar es Salaam.
Naibu Waziri Wizara ya Katiba na Sheria Jumanne Sagini akifuatilia Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria kwa Mkoa wa Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Eliakim Maswi akisalimiana na viongozi wa dini wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria kwa Mkoa wa Dar es Salaam.
Vijana wa Bodaboda wakiandamana wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Mkoa wa Dar Es Salaam.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akipata malezo kutoka kwa wataalamu wa Wizara ya Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar alipokua akikagua mabanda ya kutolea huduma mbalimbali Juni 16 2025 katika uwanja wa Maturubai Mbagala wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kwa mkoa wa Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akipata nakala ya kipeperushi katika banda la Wizara ya Katiba na Sheria wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kwa mkoa wa Dar es Salaam