Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Katiba na Sheria

Kitengo cha Ununuzi na Ugavi

Malengo:

Kutoa huduma za kitaalamu katika manunuzi, uhifadhi na huduma za ugavi.

kitengo hiki kitatekeleza shughuli zifuatazo:

 

  1. Kuandaa Mpango wa Manunuzi wa Mwaka wa Wizara.
  2. Kushauri menejimenti kuhusu masuala yanayohusu manunuzi ya bidhaa na huduma na usimamizi wa vifaa.
  3. Kufuatilia uzingatiaji wa mchakato na taratibu za manunuzi kwa mujibu wa sheria ya manunuzi ya umma.
  4. Kununua, kutunza na kusimamia vifaa na huduma za ugavi ili kusaidia mahitaji ya ugavi wa wizara.
  5. Kufuatilia usambazaji wa vifaa vya ofisi.
  6. Kudumisha na kuhuisha orodha ya bidhaa na vifaa.
  7. kutoa huduma za sekretarieti kwa bodi ya zabuni ya wizara kwa mujibu wa sheria ya manunuzi ya umma.
  8. kuweka vipimo/viwango vya bidhaa na huduma zinazonunuliwa na kufuatilia thamani ya fedha.