Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Katiba na Sheria

Chana Ashiriki Maadhimisho ya Mashujaa wa Vita ya Kwanza ya Dunia

Imewekwa: 13 Nov, 2023
Chana Ashiriki Maadhimisho ya Mashujaa wa Vita ya Kwanza ya Dunia

Na Lusajo Mwakabuku - WKS DSM

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ameshiriki Ibada ya maadhimisho ya siku ya Mashujaa waliopoteza maisha wakati wa Vita ya Kwanza ya Dunia iliyofanyika kwenye makaburi ya Jumuiya ya Madola Kijitonyama, tarehe 12 Novemba, 2023 Jijini Dar es salaam.

Akizungumza kwenye maadhimisho hayo yaliyoandaliwa kwa ushirikiano baina ya Ubalozi wa Uingereza na Ubalozi wa Ujerumani Waziri Chana amesisitiza kuwa Tanzania itaendelea  kuhamasisha Jamii na Nchi mbalimbali kuitunza na kudumisha amani.

Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa Duniani hufanyika kila Jumapili ya kwanza baada ya Novemba 12 kila mwaka kwa lengo la kuwakumbuka na kuwaombea mashujaa waliopoteza maisha kwenye Vita ya Kwanza ya Dunia.