Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Katiba na Sheria

Dkt. Chana Atembelea Chuo cha Uanasheria kwa Vitendo

Imewekwa: 18 May, 2024
Dkt. Chana Atembelea Chuo cha Uanasheria kwa Vitendo

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana leo Mei 18, 2024 Jijini Dar es Salaaam amefanya kikao na Uongozi wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo  (Law School of Tanzania) ukiongozwa Prof. Sist J. Mramba Kaimu Mkuu wa Taasisi hiyo ili kujadili  kanuni na taratibu mbalimbali za uendeshaji Taasisi na kuona namna ya  kuboresha kanuni hizo ili kukuza ufanisi katika mafunzo ya uanasheria kwa Vitendo.