WANAWAKE DODOMA WANUFAIKA NA HUDUMA ZA MSAADA WA KISHERIA
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, ameipongeza Wizara ya Katiba na Sheria kwa juhudi za kuwasaidia wanawake kupata haki zao kupitia kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia.
Mhe. Senyamule ametoa pongezi hizo leo tarehe 8 Machi 2026 katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambapo katika mkoa wa Dodoma kilele cha Maadhimisho hayo kimefanyika katika Wilaya ya Kongwa.
Mhe. Senyamule amesema kuwa jitihada zilizofanywa na wizara kwa nchi nzima zinaashiria dhamira ya Serikali ya kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi hususani Wanawake na inasaidia kuongeza uelewa wa masuala ya kisheria na kutoa fursa kwa wanawake kushughulikia changamoto mbalimbali za kisheria zinazowakabili katika jamii.
Katika maadhimisho hayo, wanawake kutoka Wizara ya Katiba na Sheria wameungana na wanawake wengine kuadhimisha siku hiyo kwa kutoa huduma ya msaada wa kisheria bila malipo kwa wananchi