Bwana Eliakim Chacha Maswi akila kiapo kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Julai 26, 2024 Ikulu Dar es Salaam.
Bwana Eliakim Chacha Maswi (mwenye maua) baada ya kupokelewa na Viongozi wa Wizara na baadhi ya Wakuu wa Taasisi za Wizara, Julai 26, 2024 Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Dar es Salaam.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Hazara Chana akiongea kwenye hafla ya kumkaribisha Katibu Mkuu Maswi, Julai 26, 2024 Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akiongea kwenye hafla ya kumkaribisha Katibu Mkuu Maswi, Julai 26, 2024 Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Dar es Salaam.
Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Chacha Maswi akiongea na Viongozi wa Wizara na baadhi ya Wakuu wa Taasisi za Wizara kwenye hafla ya kumpokea kama Katibu Mkuu mpya, Julai 26, 2024 Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu akielezea kwa kifupi majukumu ya Wizara kwenye hafla ya kumkaribisha Katibu Mkuu Maswi, Julai 26, 2024 Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Dar es Salaam.
Bwana Eliakim Chacha Maswi (wa pili kulia) kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa Wizara na baadhi ya Wakuu wa Taasisi za Wizara baada ya kupokelewa, Julai 26, 2024 Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Dar es Salaam.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (katikati) kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maveterani waliopigana vita ya Uganda wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa kwenye Viwanja vya Mashujaa eneo la Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma. Mgeni Rasmi katika Maadhimisho hayo alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Julai 25, 2024.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi. Dkt. Pindi Chana alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Switzerland aliyemaliza muda wake nchini Tanzania Bw. Didier Chasot. Julai 22, 2024 Dar es Salaam.
Balozi wa Switzerland aliyemaliza muda wake nchini Tanzania Bw. Didier Chasot akifanya mazungumzo na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi. Dkt. Pindi Chana. Julai 22, 2024 Dar es Salaam.